
Borussia Dortmund
wamewapoteza wachezaji watatu nyota lakini kocha Thomas Tuchel anasema
anataraji kuwa na mwanzo mpya na kuwapa wapinzani wao Bayern Munich ushindani
mkali katika msimu mpya
Borussia Dortmund walimaliza
wa pili katika ligi kuu ya kandanda Ujerumani - Bundesliga na wakafika fainali
ya Kombe la Shirikisho la Kandanda Ujerumani - DFB Pokal msimu uliopita lakini
kocha Thomas Tuchel anatumai kuwa na mwanzo mpya katika msimu ujao wa
Bundesliga wakati kikosi chake kinawakosa wachezaji kadhaa wa zamani nyota.
Tuchel anaendelea na
maandalizi ya msimu mpya bila beki Mats Hummels na wachezaji viungo Ilkay
Guendogan na Henrikh Mkhitryan, ambao wote wameuzwa.
Lakini Dortmund, baada ya
kuwapoteza wachezaji hao, ilijitahidi kuitumia vyema hali hiyo. Klabu
ilikusanya zaidi ya euro milioni 100 kutokana na uuzaji wa nyota hao watatu na
ikajitosa katika soko la ununuzi wa wachezaji kwa kutumia euro milioni 60.
Beki wa Ureno iliyoshinda Kombe
la Ubingwa wa Ulaya 2016, Raphael Guerreiro, beki Marc Bartra, viungo Sebastian
Rode, Ousmane Dembele na Mikel Merino, na mshambuliaji Emre Mor wote watajiunga
na kikosi hicho wakitaraji kutoa ushindani mkali kwa Bayern ili kuizuia kutwaa
taji la tano mfululizo la Bundesliga.
Kikundi cha wachezaji hao
waliosajiliwa, ni chipukizi wote na Tuchel anasema anatumai watafanya vyema
maana hawakuwa na njia nyingine. Wanaweza kuiga mfano wa Pierre-Emerick
Aubameyang na Marco Reus ambao wanafanya vyema katika timu hiyo.
Post a Comment