SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Wales yatupwa nje ya mashindano.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Wachezaji wa zamani wa Manchester united waibeba ureno. Na Charles Kunji Timu ya taifa ya Wales imekubali kichapo cha goli ...
Wachezaji wa zamani wa Manchester united waibeba ureno.



Na Charles Kunji


Timu ya taifa ya Wales imekubali kichapo cha goli 2-0 dhidi ya timu ya taifa ya ureno katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza wa kombe la euro linalofanyika huko nchini ufaransa.
Goli la kwanza la timu ya taifa ya ureno, lilifungwa na nahodha wa timu hiyo, mshambuliaji wa kimataifa anayekipiga katika timu ya Real Madrid C. Ronaldo, dakika ya 50 akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Rafael Guameiro wakati goli la pili likifungwa na Lous Nani dakika ya 53 akimalizia pasi murua ya Ronaldo.
Wafungaji wa magoli wote walishawahi kukipiga katika klabu ya Manchester United kwa mafanikio kadhaa na baadae wote wakatimkia mahala pengine kwa ajili ya kutafuta maisha mengine ya mpira. Wakati Ronaldo akiendelea kukihudumu kikosi cha Real Madrid, Nani yeye amesaini mkataba wa miaka mine kuihudumu klabu ya Hispania, timu ya Valencia.
Pamoja na Wales kutumia mbinu tofauti, huku wakimtegemea mchezaji wao tegemezi Gareth Bale aliyekuwa akihaha uwanja mzima kujaribu kuibeba Wales, bado haikusaidia kitu mbele ya nyuso za akina Renato Sanchezi, Nani Ronaldo na wengineo waliokuwa na nia ya kuhakikisha wanaipeleka timu yao hatua ya fainali.
Ronaldo amewafikia akina Payet, Bale, Giroud wote wakiwa na magoli matatu huku Antonio Greezman akiongoza kwa jumla ya magoli manne.
Lakini pia ni kitu kizuri kwa ronaldo goli la kichwa alilofunga limefikia idadi ya magoli 9 rekodi aliyokuwa anaishikia mchezaji wa zamani  Michel Plattin na kumpa hamasa endapo atapata goli katika mchezo wa fainali utamfanya kuivunja rekodi hoyo na kuweka rekodi yake.
Kwa timu ya Wales, haya ni mafanikio makubwa kwao kwani tangu mwaka 1958 walikuwa hawajafuzu matika mashindano yeyote makubwa na kufuzu kwao euro mwaka huu mpaka kutolewa hatua ya nusu fainali ni mafanikio makubwa kwao na kuweka rekodi nyingine.


Wales itawasubiri kati ya timu ya ufaransa au ujerumani itakayofungwa kwa ajili ya kutafuta mshindi wa tatu kabla ya kupisha fainali ya kumtafuta bingwa wa ulaya.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top