SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Je, wamjua Zlatan Ibrahimovic?
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
      Je, wamjua Zlatan Ibrahimovic? Hakuna kitu kingine ambacho kimekuwa kikituunganisha walimwengu wote kama mchezo wa soka n...
      Je, wamjua Zlatan Ibrahimovic?




Hakuna kitu kingine ambacho kimekuwa kikituunganisha walimwengu wote kama mchezo wa soka na bila kujijua tumekuwa tunawafaham watu wengi ambao pengine ni nadra sana kukutana nao uso kwa uso.
Pamoja na Sanaa nyingine kadha wa kadha ikiwemo miziki, siasa, michezo mbalimbali ya kuigiza, mpira wa kikapu, masumbwi itupelekeayo kuwafahamu watu mbalimbali wa kimataifa, mchezo wa mpira wa miguu umetuunganisha na ulimwengu mzima na kujihisi sasa kama tupo wote sehemu moja na pengine kujihisi hata tunaweza kuwa tukipiga stori  kwa ukaribu Zaidi kumbe la, hasha.
Ukikaa kwenye vikundi vya watu mbalimbali, mkawa mnapiga soga za hapa na pale za kimichezo, mkawa mnawatafuta wanadinga walioonyesha vipaji vya hali ya juu, wakati unawataja akina Diego Almando Maradona, Emmanuel Pettit, TIELY Henry, Luis Figo, Yohan clayff pamoja na akina Zinedine Zidane wa kizazi hicho, lakini pia ukawakumbuka akina Lionel Messi, Adjen Robben, Christian Ronaldo, hakika ni makosa sana kumsahau Zlatan Ibrahimovic akifahamika kwa jina la Ibra Kadabla.
Zlatan Ibrahimovic mwenye umri wa miaka 34 na urefu wa mita 1.95 akicheza kama mshambuliaji namba 9 alizaliwa mnamo tarehe 3 ya mwezi wa kumi mwaka 1981, Malmo, huko nchini Sweden.
Akiwa anatarajiwa kuihudumu klabu ya Manchester united msimu ujao baada ya kusajiliwa kwa uhamisho huru kutoka klabu ya PSG, Kadabla kariya yake ya soka alianza katika timu ya malmo akiwa na timu ya vijana na kufanya vyema sana na kupandishwa katika timu ya wakubwa mwaka 1999.
Aliweza kuitumikia Malmo kwa miaka miwili kabla ya kufanya uhamisho kwenda klabu ya nchini uholanzi timu ya Ajax ambapo hapo alidumu kwa miaka mitatu. Mwaka 2004 alisajiliwa na timu ya Juve ya nchini Italy kwa uhamisho wa Euro 16m. Napo hapo hakudumu pia na kusajiliwa na klabu ya Inter kwa gharama ya euro 24.8mil.
Bado safari ya kadabla ilikuwa inaendelea. Pamoja na kufanya makubwa akiwa na Inter, bado alikuwa na hamu ya kuendelea kupata changamoto nyingine kutoka vilabu tofauti na katika mwaka wa 2009 alisajiliwa na klabu ya FC Barcelona kwa uhamisho ghari Zaidi wa Euro 68.50mil na akiwa klabuni hapo alifanikiwa kutwaa kombe la ligi ya mabingwa barani ulaya huku wakichukua na kombe la ligi ya Hispania. Napo Barcelona hakudumu sana na hivyo kusajiliwa na AC Milan kwa mkopo. Mwaka 2011 uhamisho wa mkopo wa Kadabla ukakomea hapo na AC Milan wakamchukua tena kwa usajili wa Euro 24milna kuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa Zaidi duniani.
Mwaka 2012 klabu ya nchini Ufaransa PSG wakavutiwa na namna ya uchezaji wa Kadabala na kumsajili kwa ada ya juma ya Euro 22mil na kufanya makubwa akiwa na PSG kama kuchukua kombe la legie 1 mara 3 na kombe la Ufaransa mara 2 huku akifunga magoli 162 akiwa na klabu ya PSG.
Mwaka huu kandarasi yake ilikuwa imefika kikomo na hivyo kuondoka klabuni hapo na kusajiliwa na timu ya Manchester United ambayo imepoteza mvuto tangu kuondoka kwa aliyekuwa mkufunzi wa klabu hiyo kwa muda hivi Sir Alex Fergason na sasa iko chini ya Jose Morinho akitegemewa kuirudisha klabu  hiyo katika enzi zake za zamani. Uwezo wa Zlatan Ibrahimovic sina shaka nao, laikini shaka yangu ni uhitaji wa United mafanikio ya haraka ambao kwangu naona laweza kuwa tatizo kwani huenda akatamani kufanya vingi, lakini umri unamvuta mkono na kumrudisha nyuma na kuwafanya mabosi wa klabu hiyo kumtimulia mbali.
     
                               

Mechi yake ya kwanza timu ya taifa ya Sweden ilikuwa ni 2001 nakuendelea kuihudumu timu hiyo bila mafanikio huku 2010 akiteuliwa kuwa nahodha mpaka anatundika daruga baada ya umri wake kumtupa mkono. Akiwa timu ya taifa, Kadabla alifanikiwa kuifungia timu hiyo magoli 62.
Huyo ni Zlatani Ibrahimovic anayetegemewa kuirudisha hadhi ya klabu ya Manchester United wakati huku umri unamtupa mkono. Japo anaweza kuonyesha mchango mkubwa lakini changamoto za vijana wenye damu change wanaotafuta jina kama akima Rashford kwake inaweza kuwa kikwazo huku changamoto ya kukutana na ugumu wa ligi ya wingereza. Kila la kheri Kadabla ukifahamu ya kuwa ile sio legie 1 tena, utakutana na akina Sauthomptom, everton Liverpool na vilabu vikubwa vinavyoweza kuumaliza uwezo wa miguu yako.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top