SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Tuzo za VPL Zamiminika Jangwani.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Pamoja na msimu wa VPL kumalizika tangu mwezi mei, ukiwa ni muda sasa umepita, leo kumetolewa tuzo za watu waliofanya vizuri na tak...



Pamoja na msimu wa VPL kumalizika tangu mwezi mei, ukiwa ni muda sasa umepita, leo kumetolewa tuzo za watu waliofanya vizuri na takribani tuzo kumi na tatu zimeweza kutolewa.  Tuzo zilizokuwa zinagombaniwa ni pamoja na mchezaji bora wa kigeni, iliyokuwa ikiwaniwa na Donald Mgoma na Thabani Kamusoko wote wa klabu ya yanga pamoja na kipa wa klabu ya Simba Vicent Agban. Thabani SIkala Kamusoko akaibuka kidedea kwa kutwaa tuzo hiyo
Zawadi ya mshindi wa nne ilikwenda kwa klabu ya Tanzania Prisons, wakati mshindi wa tatu akiwa ni Simba na mshindi wa pili akiwa Azam FC huku mabingwa wa VPL wakiwa ni klanu ya Young Africans wao wakijiita wa kimataifa.
Zawadi ya mfungaji bora ilikwenda kwa mchezaji wa kigeni anayekipiga klabu ya Young African kutoka nchini Burundi AmisiTambe aliyefunga magoli 21 mbele ya Hamis Kiiza aliyekuwa na magoli 19.
Kocha bora wa msimu alikuwa nim kocha wa klabu ya Young Arican Hans Van Pluijm aliyewapiku wenzake wote na kutwaa tuzo hiyo ikiwa ni mara yake ya kwanza.
Tuzo ya goli bora ilikuwa inawaniwa na Amis Tambwe pamoja na Ibrahim Ajib Migomba wa Simba aliyekuwa na magoli mawili na Migomba kuibuka na tuzo hiyo kwa goli alilolipata wakati walipocheza na klabu ya Mgambo JKT.
Tuzo ya mcheza bora wa mwaka ilikuwa ipambanishwa na akina  Shiza Kichuya aliyekuwa mtibwa na kuweza kusajiliwa na klabu ya Simba, Juma Abdul Mnyamani pamoja na Muhamed Hussein na Tuzo hiyo kuchukuliwa na Juma Abdul Mnyamani.

Tuzo nyingine zilizotolewa usiku huu ni pamoja na mwamuzi bora iliyochukuliwa na Ngole Mwangole, Timu yenye nidhamu wakati Mtibwa Sugar wakinyanyua tuzo hiyo huku tuzo nyingine ni ile ya mchezaji bora chipukizi iliyochukuliwa na mchezaji wa Simba Muhamed Hussein Zimbwe Junior huku kipa bora akiiubaki Aishi Manulla wa klabu ya Azam fc
Kwa mahesabu ya haraka haraka, kati ya tuzo 13 zilizokuwa zinagawiwa, tuzo 5 zimechukuliwa na klabu ya yanga tuzo hizo zikiwa ni kocha bora, mchezaji bora, mfungaji bora, mchezaji bora wa kigeni pamoja na timu kuchukua ubingwa.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top