SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Ronaldinho: MESSI Bado ni Mchezaji Bora Duniani.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
. Ronaldinho Gaucho amesema, Lionel Messi bado ni mchezaji bora duniani licha ya kushindwa kuipatia timu yake ya taifa ya Argentina ma...
Lionel Messi retired from Argentina duty last month


.
Ronaldinho Gaucho amesema, Lionel Messi bado ni mchezaji bora duniani licha ya kushindwa kuipatia timu yake ya taifa ya Argentina mataji makubwa duniani.
Messi 29, ni mfungaji bora katika nchi yake akiwa ameifungia Argentina magoli 55, amestaafu kucheza kimataifa mwezi uliopita baada ya kukubali kupoteza fainali ya Copa Amerika dhidi ya timu ya taifa ya Chile kwa miaka miwili mfululizo.
Messi ambae ameshinda taji la  Ballon d'Or mara tano, amecheza fainali ya Copa America mara tatu na fainali ya kombe la dunia mwaka 2014 na kuweza kupoteza mataji yote.
Cristiano Ronaldo hivi karibuni ameshinda kombe la EURO akiwa na timu yake ya taifa ya Ureno, na hivyo kuibua mjadala mzito ya kwamba kati yao wote wawili, ni nani mchezaji bora Zaidi ya mwenzake lakini Ronaldinho ambae alifanikiwa kushinda kombe la dunia mwaka 2002 na timu ya Brazil, anaamini kwamba Messi aliyekuwa mchezaji mwenzake wakati wapo timu ya Barcelona ni bora Zaidi.
‘‘Kwangu mimi, Messi kustaafu soka kimataifa, haibadilishi kitu” Gaucho alisema.
‘‘Bado ni mchezaji bora wa dunia, heshima niliyonayo kwake, haibadiliki kamwe” ‘‘Na kama kweli ameamua kustaafu kuichezea timu ya taifa, basi wanamichezo watakosa uwepo wake na mashabiki kwa ujumla”
Ronaldinho Gaucho aliyewahi kushinda tuzo ya Ballon d'Or mwaka 2005, kipindi cha miaka mitano kabla ya kuachiwa na Barcelina, amesema alikuwa anamlea Messi wakati wanacheza wote Nou camp na anaamini ya kuwa Mwargentina huyu amekuwa ni mwongozo kwa akina Neymer kwa kipindi chote na kuisadia timu yao kutwaa mataji.
‘‘Japo nipo mbali nisiweze kuona kinachoendelea klabuni hapo, lakini mwangozo na ujumbe niliokuwa nao mimi kwa Messi, ndio kitu hicho hicho anachokifanya Messi kwa Neymer kwa sababu ni muhimu sana kwa mchezaji mzoefu kushare vitu tofauti na wachezaji wachanga” Gaucho alifafanua.
Ronaldinho played with Messi at Barcelona

Na Gaucho akamalizia akisema, ‘‘NA hicho ndicho kitu kikubwa sana kilichompelekea Neymer kuzoea mfumo wa Barcelona na kufiti kama walivyokuwa yeye [Gaucho] na Messi.
Huo ni mtazamo wa aliyekuwa mchezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona ya nchini Hispania, akiwa anaamini bado Ronaldo si kitu mbele ya Messi alivyokuwa akihojiwa na skyspot. Wewe mtazamo wako uko wapi kati ya hawa mabwana wawili, Ronaldo anastahili kuitwa mchezaji wa dunia, kama ni ndio, unathibitisha jibu lako kwa vigezo gani, na kama ni kinyume na hayo, pia unatumia vigezo gani?



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top