
Katibu Mkuu wa klabu ya Simba SC Patrick Kahemele
amekiambia kituo kimoja cha radio cha jijini Dar es Salaam kwamba, kutemwa kwa
mshambuliaji raia wa Uganda Hamisi Kiiza kumetokana na nidhamu yake mbovu ndani
ya klabu hiyo.
Kahemele amesema kamati ya usajili ya Simba imeamua
kuachana na mshambuliaji huyo baada ya kukaa nae mara kadhaa lakini hakukuwa na
mabadiliko ndipo walipoamua kuchukua uamuzi wa kuachana naye.
“Mchezaji akianza kuleta maneno maneno au akianza
kufanya vurugu inakuwa shida na inaweza kuharibu timu nzima. Na mwaka huu Simba
imepania kufanya vizuri kwahiyo haiwezi kuruhusu virusi ndani ya klabu,” aesema
Kahemele ambaye ameanza kutekeleza majukumu yake kama Katibu Mkuu wa Simba
tangu Julai mosi alipotambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari.
Kiiza aliifungia Simba magoli 19 magoli mawili
nyuma ya Amis Tambwe mfungaji bora wa msimu uliomalizika na kuisaidia timu yake
kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa VPL nyuma ya Azam FC na
mabingwa wa ligi hiyo Yanga SC.
Post a Comment