
Wakati vilabu vikijiandaa rasmi kwa msimu mpya wa ligi, haswa
zile timu kubwa zilizokutana kule nchini china nao wachezaji hawako nyuma, kila
mmoja anatafuta staili yake itakayokuwa na mwonekano tofauti kwa mashabiki wake
ili tu kuweza kuwavutia au hata kuonekana tofauti na siku zote.
Ukiwa kama mchezaji, hutakuwa na mabadiliko makubwa sana hasa
wengi huwa wanajaribu kuonyesha utofauti kwenye style mbalimbali za unyoaji wa
nywele mifano mizuri ni kama tulivyoweza kumzoea Kiungo mshambuliaji wa klabu
ya Manchester United Maluan Fellain kwa kufuga nywele nyingi wakati wachezaji
wengine huwa wanapenda kuweka style mbalimabali ili tu kuonyesha utofauti haswa
wawapo uwanjani.

Hayo yote yakiwa yanaendelea, nae mchezaji bora mara tano wa
Ballon D ‘or Lionel Messi naye ameamua kutafuta style yake ambayo huenda
itawavutia mashabiki wake au laa.
Kama ulipitwa na
baadhi ya picha zake Messi walipokuwa safarini kwenda nchini England kucheza
huko watakapokuwa na michezo ya kirafiki, hizi ni baadhi ya picha zake.
Post a Comment