
Ikiwa ni wakati maridhawa kwa vilabu vinavyoshiriki ligi kuu
Tanzania bara kijifua kabla ya msimu mpya kuanza, Timu kadha wa kadha zimekuwa
zikitafuta maeneo tulivu kwaajili ya kuweza kuvinoa vilabu vyao kabla ya kuanza
rasmi kwa msimu mpya wa 2016-2017 unaotarajiwa kuanza rasmi tarehe 20 ya mwezi
Agosti.
Wakati hayo yakiendelea, Vilabu viwili, Mbeya city na Mtinwa
sugar vimekubaliana kucheza mchezo wa kirafiki utakaofamyika katika uwanja wa
Jamhuri jijini Morogoro tarehe 30 ya mwezi huu, jumamosi ya mwisho ya mwezi wa saba.
Taarifa kutoka uongozi wa Mbeya City pamoja na ule wa Mtibwa Sugar inasema, Kwa mujibu wa kiongozi wa Kanisa la Faith Baptist, Mch Jerry
Wyatt ambaye ndiye mwandaaji na msimamizi mkuu wa mchezo huo, amesema
maandalizi yote ya mechi hiyo ya kirafiki itakayoambatana na tamasha kubwa la
mahubiri ya neno la Mungu tayari yamekamilika ikiwa ni pamoja na timu zote
kuthibitisha kuhudhuria.
‘‘Maandalizi yote yamekamilika, timu zote zimethibitisha
kushiriki katika mchezo huo ambao utaambana na mahubiri ya neno la Mungu kwenye
uwanja wa Jamhuri, naomba watu wajitokeze kwa wingi kuja kushuhudia mchezo
mzuri wa kirafiki kutoka kwa timu hizi mbili pia kupata mahubiri mazuri ya neno
la Mungu pasipo kiingilio chochote kwa watakaofika kwenye uwanja wa Jamhuri”
Hii inakuwa ni mara ya pili kwa Mtibwa sugar na Mbeya City
kucheza mchezo wa kirafiki ulioandaliwa na Kanisa hilo awali ikiwa ni msimu
uliopia ambapo timu hiyo kutoka Manungu iliibuka na ushindai wa bao 1-0
lililofungwa kipindi cha pili na Mohamed Ibrahim
City inatarajia kuondoka Mbeya Julai 28 tayari kwa mchezo huo
uliopangwa kupigwa siku jumamosi ya mwisho wa mwezi huu.
Post a Comment