
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Chelsea ya Uingereza Demba Ba amesema
hataacha kucheza soka hata baada ya kuvunjika mguu.
Ba, ambaye kwa sasa anachezea Shanghai Shenhua ya China,
alivunjika mguu baada ya kukabwa akicheza mechi ya Ligi Kuu ya china maarufu
kama super cup.
Baada ya mechi hiyo, mkufunzi wa mshambuliaji huyo wa Senegal
Gregorio Manzano alisema jeraha hilo “huenda likafikisha kikomo uchezaji wake”.
"Hili ni jeraha mbaya sana lakini ninaweza kujikwamua.
Sitafikisha kikomo uchezaji wangu hapa, hilo nina uhakika nalo,” amesema Ba,
mwenye umri wa miaka 31.
“Msimu unamalizika Novemba na kuanza Machi. Nitajizatiti kurejea
kwa wakati kwa msimu utakaofuata.”
Demba Ba alichezea West Ham, Newcastle na Chelsea katika Ligi
ya Premia. Alijiunga na Shenhua kutoka klabu ya Besiktas ya Uturuki,
akinunuliwa takriban pauni 12 milioni mwezi Julai mwaka jana.
Kwa sasa, ndiye
mfungaji mabao bora Ligi Kuu ya Uchina akiwa na magoli 14 kutoka mechi 18.
Post a Comment