Mchezaji huyo mwenye
umri wa miaka 25 alifunga mabao 21 katika mechi 34 msimu uliopita na kandarasi
yake katika klabu hiyo inakamilika mwaka 2019.
Katika taarifa yake
katika mtandao wa Twitter, Klabu hiyo ya Ufaransa ilisema Lacazette hanunuliki
na ni miongoni mwa viongozi wa timu hiyo ya kocha Bruno Genesio.
Lyon ilikana ripoti ya
gazeti moja kwamba ilikataa ombi la Euro milioni 48 kutoka kwa klabu hiyo ya
Uingereza.
Mpaka sasa kocha wa washika bunduki wa London, Mfaransa,
Arsene Wenger amekwishakamilisha usajili wa Granit Xshaka na Takuma Asano kinda
raia wa Japan.
Post a Comment