Kipa chipukizi wa Man City Angus Gunn, 20, aliokoa mkwaju wa
penalti wa Mikel Morino na kuwahakikishia vijana wa Pep ushindi wa mabao 6-5.
Mechi hiyo iliyochezwa katika uwanja wa Longgang ulioko Shenzhen
ilikuwa imeishia sare ya 1-1 katika muda wa kawaida.
Sergio Aguero alikuwa ameiweka Man City kifua mbele
mapema katika mechi hiyo lakini mshambuliaji chipukizi wa Dortmund Christian
Pulisic, mwenye umri wa miaka 17, akawasawazishia wajerumani hao katika muda wa
majeruhi.
Hii ndio ilikuwa mechi yao ya pili baada ya ile ya kwanza kwa
Man City kupoteza mbele ya Bayern Munich kwa goli 1-0, baada ya mechi iliyokuwa
imepangwa awali dhidi ya vibonde wao wa jadi kutoka Uingereza Manchester United
kuahirishwa kufuatia mvua kubwa iliyonyesha mjini Beijing.
Post a Comment