SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Fernando Santos Ajifunga Kitanzi Mpaka 2020.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Chama cha Soka cha Ureno-FPF kimetangaza kumuongeza mkataba kocha Fernando Santos mpaka 2020 baada ya kukiongoza kikosi cha timu ya taif...
Fernando Santos


Chama cha Soka cha Ureno-FPF kimetangaza kumuongeza mkataba kocha Fernando Santos mpaka 2020 baada ya kukiongoza kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo kutwaa taji la michuano ya Ulaya mwaka huu kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wenyeji Ufaransa.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 61, ambaye amekuwa akikinoa kikosi hicho toka Septemba mwaka 2014, aliiongoza Ureno kutwaa taji lake la kwanza kubwa la kimataifa pamoja na kucheza bila nyota wake Cristiano Ronaldo katika fainali dhidi ya wenyeji Ufaransa mapema mwezi huu.
Mkataba wake mpya alioongezwa utamfanya kukiongoza kikosi hicho katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na ile ya mataifa ya Ulaya. Timu ya taifa ya Ureno itaanza kampeni zake katika harakati za kufuzu fainali za kombe la dunia za mwaka 2018 za huko Urusi na timu ya taifa ya Switzerland tarehe 6 septemba.
Santos amewahi kufundisha klabu kubwa nchini Ureno zikiwemo Benfica, Sporting Lisbon na Porto huku pia akiwahi kuinoa timu ya taifa ya Ugiriki.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top