
David
Moyes ametangazwa rasmi kuwa kocha mkuu wa klabu ya Sunderland.
Moyes
53, aliwahi kuzifundisha timu kama vile Everton pamoja na
Manchester United, amekubali kibarua hicho kwamkataba wa miaka minne
kwa kipindi chote atakachokuwa hapo Light stadium.
‘‘Nimekubali
kuichukua klabu kubwa hapa England, na sapoti kubwa toka kwa wadau
wangu, na ninachokitazama sasa, kurudi upya tena nchini England kwa
ajili ya kufanya kazi.” Alisema Moyes.
Moyes
raia wa Scotland, amekuwa nje tangu alipotimuliwa na klabu ya Real
Sociadad ya nchini Hispania mwezi Novemba.
Moyes amekuja kuziba Pengo la Big Sam aliyekuwa kocha mkuu wa
Sunderland, aliyetangazwa rasmi kuwa kocha wa England, kufuatia kujiuzulu
kwa Roy Hogson baada mashindano ya EURO yaliyomalizika julai.
Mwenyekiti
mkuu wa klabu ya Sonderland, Ellis Short amesema, hata hivyo Moyes
alikuwa kwenye mipango yake muda mrefu sana wa kuwa kocha wa paka
weusi, Sunderland.
‘‘Ni
mtu ambae historia yake ya mpira inajieleza na ni mtu ambae muda
mwingi nimekuwa nikitamani awe klabuni hapa”alisema Short.
‘‘Nimezungumza naye mambo kadha wa kadha, na nimevutiwa sana
naye” alimalizia Short.
Moyes
alianza kariya yake kama kocha na klabu ya Preston huko kaskazini
mwisho na alikwisha wahi kupigiwa kura mara tatu kwenye tuzo za kocha
bora miaka kumi na moja kabla ya kutimuliwa na klabu ya Everton.
Alichukua
nafasi ya Mscotish mwenzake, Sir Alex Ferguson, aliyeiongoza klabu ya
Manchester United kwa jumla ya miaka 26 kwa mafanikio makubwa.
Lakini
licha ya kusaini kandarasi ya miaka 6 ndani ya Traford,
alifukuzwa baada ya miezi kumi kwa kuipelekea timu kutokuwa na mataji
na hivyo kutimkia Real Sociadad ya nchini Hispania kumpisha aliyekuwa
kocha wa timu ya taifa ya Uholanzi Louis Van Gaal.
Moyes
alikuwa anahusishwa kuifundisha klabu ya Aston villa iliyoshuka daraja
nsimu uliopita, lakini akajitoa mwenyewe kwa kuwatosa na nafasi hiyo
kuchukuliwa na Dimatheo.
‘‘Ninachokitazama
kwa sasa, ni kufanya kazi nzuri iliyokuwa ikifanywa na BIGSAM”
Alisema Moyes.
Post a Comment