
Ligi kuu ya EPL kwa msimu utakaoanza mnamo tarehe 13 ya mwezi
ujao, kuna sura kadha wa kadha ambazo si ngeni sana machoni pa wapenda soka,
lakini pengine ugeni utajitokeza pale katika ligi hiyo maarufu sana duniani.
Sura za akina Morinho zimekwisha zoeleka kwani kocha huyo maarufu sana
ulimwenguni alikwishawahi kufanya kazi na klabu ya Chelsea pamoja na Real
Madrid ya nchini Hispania lakini pia hata ule wakati anachukua kombe la klabu bingwa
barani ulaya akiwa na klabu ya Inter ya nchini Italia.
Tuachane na hayo, mahasimu wawili Pep Guardiola pamoja na
Jose Morinho watakuwa wakivinoa vilabu vya jijini Manchster, Morinho akiwa kwa
mashetani wekundu wakati Guardiola atakuwa upande wa pili wa shilingi akikinoa
klabu cha Manchster City vyote vikiwa katika mji mmoja na waswahili wengi
huvitofautisha kwa kuvipa majina ya MU ni ya kijijin wakati M/city ni ya mjini.
Siku zikutanapo timu hizi katika ligi kuu huwa ni DABI iliyobeba
hisia mbalimbali haswa kwa kila nafasi ya klabu moja moja lakini pia hata
historia ya timu hizo kubwa sana duniani.
Mwaka huu, utamu wa mechi hiyo unanogeshwa Zaidi na uwepo wa
hawa makocha wakubwa na historia zao Guardiola pamoja na Morinho na hivyo DABI
kuhama toka kwenye timu mpaka kwa wakufunzi. Nani Zaidi ya mwenzake, ni swali
ambalo mimi na wewe, tutakosa majibu mazuri sana ya ushawishi kwa watu Zaidi ya
kusema tukae na tusubiri mpaka wakati mwafaka tutakapoona picha halisi ya kila
kocha na nafasi ya timu yake.
Mara ya mwisho Pep Guardiola na Jose Morinho kusalimiana kwa
kushikana mikono ni kile kipindi wakati Guardiola akiifundisha klabu ya
Barcelona wakati Morinho akiwafundisha mahasimu wao wakubwa klabu ya Real
Madrid kile kipindi kuanzia mwaka 2010-2012 kabla ya kila mmoja hajatimkia
kwake.
Hii ni Zaidi ya DABI
ya jiji la Manchester wanapokutana mafahari hawa wawili na kipimo kikubwa
kinaanza hapo siku ya kesho watakapokutana katika michezo ya kujiandaa na msimu
ujao inayofanyika huko nchini China.
Manchester United wanakutana na Manchester city huku Morinho
akiwa amejeruhiwa vilivyo na klabu ya BVB ya nchini Ujerumani kwa magoli 4-1
mchezo uliofanyika siku ya alhamisi.
Kuelekea mchezo wa hiyo leo, kila kocha ameonyesha kutokuwa
na hofu na kocha mwenzake na haya aliyaongea Morinho wakati walipotua njiani
baada ya ndege yao kukutana na anga iliyokuwa haijatulia na hivyo kuweza
kuahirisha safari yao kuelekea mji wa Shanghai.
Kwa upande wa shilingi, nae Guardiola ameonyesha kutokuwa na
uadui na kuweza kuthibitisha ya kuwa Morinho ni rafiki yake mkubwa na walisha
wahi kufanya kazi nae sehemu moja, kwahiyo kumsalimia kwa kumpa mkono kwake
wala sio zoezi gumu kiasi hicho walichokuwa wanakifikiri waandishi wengi wa
habari za michezo.
Safari ni ndefu wakati Morinho ni sawa na fisi aliyepewa
mfupa mzito kuutafuna na wakati huo hajala siku nzima, kwake ni zoezi ambalo
pengine linaweza kuwa tatizo kubwa sana wakati Guardiola atahitaji uvumilivu wa
hali ya juu kutoka kwa mashabiki wa M/city ili kuweza kupandikiza falsafa zake
kuliko kushikiwa bango kutaka matokeo ya haraka.
Post a Comment