SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: lallana atoa neno kuelekea mechi ya wales na uingereza.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Picha na goal.com Uingereza walilazimishwa sare ya uzembe na Urusi katika mechi ya awali, sasa wanalazimika kushinda dhihdi ya Wales ...

Lallana: Ni ujinga Uingereza kumchunga Bale
Picha na goal.com
Uingereza walilazimishwa sare ya uzembe na Urusi katika mechi ya awali, sasa wanalazimika kushinda dhihdi ya Wales ili kujiweka katika mazingira mazuri
Adam Lallana amesisitiza kuwa Uingereza watakuwa wajinga wa mwisho iwapo wataelekeza nguvu zao zote kumkaba Gareth Bale watakapoikabili Wales katika mechi ya Euro 2016 Alhamisi.
Wales wanaweza kutinga hatua ya mtoano kama watashinda mechi nyingine, na nafasi yao kusonga mbele ni kubwa zaidi kwa kumtegemea supastaa wa Real Madrid Gareth Bale.
Hata hivyo Lallana ameelezea ubora wa kikosi cha Chris Coleman na amesisitiza kuwa umakini unahitajika katika mechi ya Alhamisi.
'Wales wana wachezaji wengi wenye vipaji kwa hiyo si Gareth Bale pekee wakuchungwa,' fowadi huyo wa Liverpool alisema.
'Joe Allen alikuwa nyota wa mchezo siku ambayo Wales walishinda dhidi ya Slovakia, na hali kadhalika Aaron Ramsey.
'Ni moja ya wachezaji bora watano duniani kwa sasa? Naam. Ni rafiki yangu sana na mchezaji mzuri sana ambaye sote tunamfahamu.  Lakini hatutamchunga Bale pekee, huo utakuwa ni ujinga.
'Sisi tunajitazama wenyewe, hatuna budi kuheshimu uimara wa Wales na kuchunguza madhaifu yao, lakini kama tukicheza kwa kujituma tutaweza kushinda kila mchezo.'

Katika mechi ya Alhamisi meneja Roy Hodgson anafikiria kumuingiza dimbani Daniel Sturridge.
Chanzo ni www.goal.com

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top