SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Hali ni ngumu uingereza, ubelgiji.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
               MAKALA YA EURO. Na Charles Kunji. picha na bbc swahili Takribani miaka 56 tangu kuanzishwa kwa mashindano ya mat...
               MAKALA YA EURO.
Na Charles Kunji.

picha na bbc swahili

Takribani miaka 56 tangu kuanzishwa kwa mashindano ya mataifa huru ya ulaya yakifahamika kama UEFA EUROPEAN NATIONS CUP. Kwa mara ya kwanza mashindano haya kushika kasi ilikuwa ni mwaka 1960, ambapo kuanzia hapo hadi sasa yameweza kufanyika mara 14 na mataifa yaliyoweza kunyanyua kwapa kuchukua kombe hilo ni mataifa tisa pekee. Mataifa hayo ni pamoja na  ujerumani na Hispania wote wakiwa wamechukua mara tatu. Ufaransa ambao ni wenyenyi wa mashindano ya mwaka huu wao wameweza kunyanyua kwapa mara mbili, mwaka 1984 na mwaka 2000 wakichagizwa na ule moto wa mwaka 1998 walipoweza kumfunga brazil 3-1 kwenye fainali ya kombe la dunia. Mataifa mengine ni soviet union [Russia], Italy, jamhuri ya cheki, uholanzi, Denmark pamoja na ugiriki ambao wote kwa pamoja wamechukua kombe hili mara moja. Kumbukumbu inatuambia kuwa, tangu kuanzishwa kwa mashindano haya, ni mataifa matatu pekee ambayo ni Hispania, italia pamoja na wenyeji wa mwaka huu ufaransa ndio wameweza kuchukua kombe hili katika ardhi ya nyumbani. Msimu wa pili wa mashindano haya ambao ni 1964, Hispania ndiye aliyekuwa mwenyeji na kuweza kuchukua kombe hilo.  Waswahili wanasema jifunze furaha ya jirani yako. Ndipo mashindano yaliyofuata katika mwaka 1968, italia akawa mwenyeji wa mashindano na kuweza kufanya kama wlivyofanya Hispania katika miaka minne iliyopita kwa kipindi hicho. Miaka 16 baadae, ufaransa akapata tiketi ya kuandaa mashindano na kuweza kuitumia vyema nafasi ya kucheza nyumbani na kuchukua kombe hilo. Nimiaka kadhaa sasa yapata umri wa wazee wetu hakuna tena taifa lililoweza kuthubutu kufanya kama walivofanya Hispania, italia pamoja na ufaransa.
Ni Hispania pekee ambao wameweza kuchukua kombe hili kwa misimu miwili mfululizo. Waliweza kufanya hivyo mwaka 2008 wakati wenyeji walikuwa ni AUSTRIA pamoja na USWISI. Safari haikuishia hapo, Hispania katika miaka hiyo walikuwa na kizazi bora kabisa kama vile CAROSY PUYOL, INIESTA pamoja na XAVI na wengineo wengi wakiongozwa na delbosk  na kombe la dunia kufanyika katika ardhi ya Africa kwa mara ya kwanza Hispania tena wakaonyesha ubora wao kwa kuchukua tena kombe la dunia kwa goli bora kabisa la kiungo iniesta. Ubabe wa delbosk uliendelea tena kwenye EURO ya mwaka 2012 iliyofanyika Poland pamoja na Ukraine ambapo Hispania tena kuchukua kombe kwa kumfunga italia magoli manne kwa 0.
Ufaransa mwaka huu wamepewa nafasi hiyo ya kuwa mwenyeji wakiwa na wachezaji kama vile hogo lrolis, mandanda, bless matuidi, ngolo kante aliyekuwa na msimu bora kabisa kwenye ligi ya uingereza, pamoja na greezman huku wakimchukua kinda ANTONIAL MARTIAL anayekipiga katika klabu ya mashetani wekundu, Manchester united huku wakimwacha nje benzima ambae anaandamwa na skendo za nje ya uwanja.  Ufaransa ambao wana kikosi kilichosheheni majina sio makubwa katika anga la kimichezo lakini wachambuzi wa soka wanaipa nafasi kubwa kwa ufaransa kufanya vizuri. Wakiwa kundi A wapo na Albania, Romania na uswisi mataifa yote yakiwa hayajawahi kuchukua kombe hili la EURO.  Baada ya mechi zote za makundi, tutakuwa tumefahamu hatma ya ufaransa. Siku si nyingi nasisi hatuchoki kusubiri tuone watakachokifanya.
Mataifa mengine ambayo watu hawayapi nafasi ya kufanya vizuri ni pamoja na ubelgiji, cratia, pamoja na mabingwa watetezi Hispania huku wingereza wakipewa nafasi finyu sana ya kutwaa ubingwa.

Niliyekuandalia Makala hii ni mimi CHARLES KUNJI mlimani radio. Elimu kwanza.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top