WALES WAIBUKA KIFUA
MBELE.

na Charles kunji
Wales ilijifurukuta na kuilaza Urusi mabao matatu kwa nunge
katika mechi ya mwisho na muhimu ya makundi jana usiku.
Aaron
Ramsey na Neil Taylor na Gareth Bale walifunga mabao hayo muhimu na kuisaidia
timu hiyo ya kocha Chris Coleman ikiwa imejihakikishia nafasi katika mkumbo wa
pili kwa mara ya pili katika historia yake.
Wales kwa mara ya
mwisho kufuzu mashibdano ya ulaya ilikuwa ni mwaka 1958 na tangu hapo wamekuwa
hawana msimu mzuri katika mashindano kadha wa kadha ya ulaya.
Amani iliwajaa tele na
nyuso za furaha tangu walipomwajili CHRIS COLEMAN alipoweza kuongoza timu hiyo
ya wales kufuzu kwenye kombe la mataifa ya ulaya.
Wales wpo kundi B
ambalo linazihusisha timu za England, Slovakia, urusi pamoja na wao
wales.wakati wales walipoweza kumaliza mechi zao tatu katika kundi B kwa
kuongoza kundi hilo kwa jumla ya pointi 7 wakiwa wameshinda mechi mbili na
kupoteza mechi moja.dhidi ya England.
Msambuliaji wa
kimataifa Gareth Bale aliiongoza timu hiyo katika ushindi wa magoli matatu kwa
sifuri nay eye akikwamisha mpira mmoja wavuni na kumfanya mchezaji aliye na
magoli mengi kwa sasa katika mashindano.
Bale anakuwa mchezaji
wa kwanza kwa wales kufunga mechi tatu mfululizo kwa takribani miaka kumi.
Post a Comment