SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: KELVIN YONDANI AMKWAZA MKWASA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
BAADA ya kikosi cha timu ya Tanzania Taifa Stars kipo nchini Nigeria tayari kwa kutupa karata yake ya mwisho ya AFCON, beki wa kla...


Image result for KELVIN YONDANI IMAGES

BAADA ya kikosi cha timu ya Tanzania Taifa Stars kipo nchini Nigeria tayari kwa kutupa karata yake ya mwisho ya AFCON, beki wa klabu ya Yanga amejiengua kwenye idadi ya watu 18 watakaocheza mchezo huo.

Taarifa ambazo shirikisho la mpira wa miguu Tanzania linazo ni kwamba Yondani anamatatizo ya kifamilia ambapo hajayaweka sawa hadi wakati timu hiyo inaondoka kwenda Nigeria.

Kocha mkuu wa Stars Charles Boniface Mkwasa amesikitishwa na kitendo hicho lakini TFF itasubiri ripoti ya kocha huyo mara baada ya kurejea kutoka Nigeria.

“Amepigiwa simu hakupokea, ametumiwa ujumbe mfupi wa maandishi lakini pia akatumiwa ujumbe kwa mfumo wa whatsapp lakini hakujibu. Tukazungumza na viongozi wa Yanga Katibu Mkuu Baraka Deus Dedit akatuambia Yondani hayupo kambini kwao na sababu ya kutokuwepo ni kwamba ametoa taarifa kwamba anamatatizo ya kifamilia”, amesema afisa habari wa TFF Alfred Lucas ambaye alizungumza na Mkwasa muda mfupi kabla ya safari.

“Jambo hilo limemsikitisha sana mwalimu (Charles Boniface Mkwasa)kwasababu ni mchezaji ambaye alimtegemea, lakini sisi kwa upande wetu  (TFF) tunasubiri ripoti ya mwalimu ndipo tuweze kuzungumza jambo au kutenda jambo.”

Stars imeondoka Dar ikiundwa na wachezaji 18 huku nahodha wake Mbwana Samatta akitarajiwa kuungana na kikosi hicho nchini Nigeria.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top