SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: BALOTELI AANZA KURUDISHA THAMANI YAKE.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
  MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Italia ambaye alitolewa bure na klabu ya Liverpool ya England kwenda klabu ya Nice ya Ufaransa, M...


 Mario Balotelli scored twice on his debut for French club Nice against Marseille


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Italia ambaye alitolewa bure na klabu ya Liverpool ya England kwenda klabu ya Nice ya Ufaransa, Mario Balotelli, amerudi kwenye headlines baada ya maisha magumu ndani ya Anfield na AC Milan ya Italia alipokuwa anacheza kwa mkopo akitokea Liverpool.
 His first came from the spot before he equalised for his side in the second half with a header


Balotelli ambaye kajiunga na Nice akitolewa bure baada ya vilabu kadhaa kutoonesha imani ya kumuamini staa huyo, amefanikiwa kupachika magoli mawili katika ushindi wa goli 3-2 dhidi ya Olympique Marsella katika mchezo wake wa kwanza kwenye klabu hiyo inayoshiriki ligin kuu ya Ufaransa.

Balotelli alitumia dakika 7 za mwanzo kuiandikia Nice goli la kwanza kwa mkwaju wa penati na dakika ya 78 alipachika goli la pili lilifanya wawe sawa na Marsella waliokuwa tayari wamewafunga goli mbili.

 Balotelli coolly rolled his penalty into the corner of the net just six minutes into his debut

Goli la tatu la Nice lililowapa point tatu na kuwafanya wapande hadi nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu Ufaransa kwa kufikisha jumla ya point 10, lilifungwa na Wylan Cyprien dakika ya 88, wakati magoli ya Marsella yalifungwa na Thauvin dakika ya 14 na Gomis kwa penati dakika ya 72.

Hata hivyo, Baloteli ametanabaisha kuwa uamuzi aliouchukua wa kujiunga na klabu ya Liverpool haukuwa uamuzi sahihi kwake na ndio maana hakuwa na furaha licha ya kushinda magoli 4 katika michezo 28 aliyocheza.

“Licha ya kuwa na mashabiki wazuri na wachezaji waliokuwa na ushirikiano na mimi lakini kiukweli sikuipenda kabisa Liverpool. Baloteli alisema muda mchache baada ya kuisha mchezo wake wa kwanza akiwa na klabu ya Nice na kuifungia goli mbili.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top