BINGWA wa VPL timu ya soka ya Yanga imeendelea na programu
zake za mazoezi kwaajili ya kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam
utakaopigwa kesho Jumatano katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaa.
Katika
mchezo huo, ambao ni maalum kwa ajili ya ufunguzi wa ligi ligi kuu, Yanga
inaenda kushuka dimbani, huku ikitarajiwa kuwakosa nyota wake kadhaa kutokana
na kusumbuliwa na majeraha yaliyotokana na michezo yao ya Kombe la Shirikisho.
Wachezaji
ambao wanatarajiwa kukosekana ni pamoja na Ally Mustafa ‘Barthez’
anayesumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu (ankle), mabeki Juma Abdul,
Andrew Vincent ‘Dante’ wanaosumbuliwa na maumivu ya miguu.
Wengine
ni Kevin Patrick Yondani anayesumbuliwa na maumivu ya jicho na kiungo
mshambuliaji Obrey Chirwa anayesumbuliwa na goti.
Mshambuliaji
tegemezi wa timu hiyo Mzimbabwe Donald Ngoma anarudi uwanjani baada ya
kukosekana kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya MO Bejaia kutokana na
kuwa na kadi mbili za njano.
Yanga
ambao pia walikuwa wakisaka tiketi ya kufuzu nusu fainali ya Kombe la
Shirikisho Afrika, wametupwa nje baada ya Medeama kuifunga TP Mazembe goli 3-2,
kwenye mchezo uliopigwa nchini Ghana juzi.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- VPL INAREJEA TENA WIKIENDI HII.01 Apr 20170
BAADA ya mapumziko ya takribani ya wiki tatu kupisha michuano mbalimbali ya kimataifa kwa ngazi...Read more »
- PLUIJM AULA SINGINDA UNITED, ASAINI KANDARASI YA MIAKA MIWILI.17 Mar 20170
BAADA ya kusambaa kwa picha kwenye mitandao ya kijamii ya aliyekuwa kocha wa zamani wa ...Read more »
- SAMATTA AZIDI KUCHANJA MBUGA ULAYA, AWEKA REKODI NYINGINE.16 Mar 20170
HII ni habari njema kwa mashabiki wa soka nchini Tanzania baada ya nahodha wa timu ya taifa...Read more »
- MWANJALI MCHEZAJI BORA WA MWEZI DECEMBER, VPL.23 Jan 20170
SHIRIKISHO la mpira wa miguu nchini, TFF limemchagua beki wa kati wa Simba, Method Mwanjale kuw...Read more »
- YANGA YAANZA NA USHINDI KWENYE MBIO ZA KUTETEA KOMBE LA FA.21 Jan 20170
RAUNDI ya tano ya mashindano ya FA [Azam Sports Federatio Cup] imeendelea leo uwanja wa Uhuru...Read more »
- BAADA YA KUTWAA MEDALI INDIA, SIMBU APEWA JUKUMU JINGINE TENA.18 Jan 20170
BAADA ya Alphonce Simbu kufanya vyema kwenye mashindano ya mbio za Mumbai Marathon, sasa cham...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.