SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: MANCHESTER UNITED YAICHAPA LEICESTER CITY.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Ligi kuu ya EPL imefunguliwa rasmi baada ya mchezo wa mabingwa wa ligi hiyo klabu ya Leicester City, The Fox kucheza na mabingwa wa k...


Ligi kuu ya EPL imefunguliwa rasmi baada ya mchezo wa mabingwa wa ligi hiyo klabu ya Leicester City, The Fox kucheza na mabingwa wa kombe la FA klabu ya Manchester United mchezo uliofanyika katika dimba la Wembley na klabu ya Manchester kuibuka na ushindi wa goli 2-1.

Mchezo huo ukifahamika kama kombe la ngao ya hisani au kwa majina ya kizungu ukiitwa, Commubity Sheald Cup, ulianza mnamo saa kumi na mbili za jioni kwa majira ya saa za Africa ya mashariki ambapo Manchester chini ya mwalimu Jose Morinho wameibuka na ushindi na hivyo kuongeza idadi ya vikombe katika hazina yao.

Klabu ya Manchester United ilikuwa imechukua kombe hili mara 20 kabla ya mchezo huu na hivyo kuongeza idadi na kuwa mara 21 huku ikiwa ni klabu pekee iliyochukua kombe hilo kuliko klabu yeyote ile.

Kwa upamde wa klabu ya Leicester, wao ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kucheza fainali hii baada ya kuwa mabingwa wa EPL msimu ulioisha.

Mchezo ulikuwa ni wa kuviziana sana na mpaka kipindi cha kwanza kinaisha, Manchester walikuwa wanaongoza kwa ushindi wa goli moja na kipindi cha pili kilivyoanza, Mshambuliaji wa Leicester, Jarmie Vardy aliisawazishia timu yake na Ibrahimovic akaweka kambani goli la pili goli la ushindi.

Kwa mchezo huo, sasa ligi kuu ya EPL imefunguliwa rasmi na mechi zitaanza wikiendi ijao.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top