![]() |
Picha na Bin Zubery |
Klabu ya wekundu wa msimbazi, Simba, leo imeadhimisha miaka
80 ya kuzaliwa kwa klabu hiyo na kucheza mchezo wa kirafiki ulioitwa jina la
Simba day dhidi ya klabu ya kutoka Kenya mabingwa wa zamani, timu ya AFC
Leopards na klabu ya Simba kuibuka na ushindi mujarabu wa goli 4-0.
Shukrani kwa magoli ya Ibrahimu Ajibu aliyefunga magoli
mawili, Shiza Kichuya pamoja na Laudit Mavugo wote wakiwa wamesajiliwa msimu
huu.

Kocha wa wekundu wa msimbazi Simba, Joseph Omog, raia wa
Cameroon, alijaribu kuwachezesha wachezaji wote, lakini kiu kubwa ya mashabiki
wa klabu hiyo ilikuwa ni kutaka kumwona mchezaji wa Burundi aliyekosa nafasi
katika klabu ya Toulouse ya nchini Ufaransa na kusajiliwa na wekundu hao wa
msimbazi ambapo,
Mavugo nae akawadhihirishia mashabiki pamoja na uomgozi wa
klabu hiyo kwamba hawakufanya makossa kumsajili baada ya kufunga goli moja na
kutengeneza nafasi moja ya goli alilolifunga Shiza Kichuya.
Kiujumla mechi ilikuwa ni ya kuvutia ambapo klabu ya Simba
walionekana kuutawala mchezo karibu dakika zote japo wapinzani wao klabu ya
Leopards walionekana kukumbuka shuka wakati kumekucha baada ya kuanza kumiliki
mpira dakika 15 za mwishoni, hata hivyo mbinu zao hazikufanikiwa na mpaka
mwamuzi anapuliza filimbi ya mwisho, ubao ulikuwa unasomeka Simba 4-0 AFC
Leopards.

Ligi kuu ya Tanzania bara inaanza rasmi tarehe 20 ya mwezi
huu na klabu ya Simba itaanza kutupa
karata yake ya kwanza dhidi ya klabu ya Ndanda ya Mtwara.
Post a Comment