SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: KAMATI YA OLIMPIC IOC YAUNDA JOPO LA WATU WATATU KWAAJILI YA URUSI.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Kamati ya kimataifa ya OLimpiki IOC imetangaza kuwa inaunda jopo la wanachama watatu ambao watatoa uamuzi wa mwisho wa wanariadha...
Olympic and Russian flag



Kamati ya kimataifa ya OLimpiki IOC imetangaza kuwa inaunda jopo la wanachama watatu ambao watatoa uamuzi wa mwisho wa wanariadha wageni wa Urusi watakaoshiriki mashindano ya olimpiki ya Rio De Jenairo huko nchini Brazil ambayo yanatarajiwa kuanza Ijumaa hii.

Msemaji wa kamati hiyo Mark Adams, ameuambia mkutano wa waandishi wa habari kuwa jopo hilo litatathmini kesi zinazowakumba wanariadha wote wa Urusi.

Jopo hilo la maafisa watatu linawajumuisha Ugur Erdener, raisi wa mchezo wa mishale , Claudia Bokel ambaye anahudumu katika jopo la Wanariadha la kamati ya Olimpiki IOC na mwakilishi wa Uhispania  Juan Antonio Samaranch ,

Kufikia sasa wanariadha 250 wa Urusi walikuwa wameruhusiwa kushiriki mashindano hayo ya Olimpiki ya Rio.

Shirika la kupambana na matumizi ya madawa ya kuongeza nguvu mwilini WADA lilikuwa limependekeza wanariadha wote kutoka Urusi wapigwe marufuku ya Kushiriki michezo yote ya kimataifa kufuatia ufichuzi uliobainisha kuwa serikali ya Urusi ilihusika katika njama ya kuficha matumizi ya madawa ya kuongeza nguvu miongoni mwa wanamichezo wake.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top