SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Ufaransa uso kwa uso na ureno.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
        Ufaransa uso kwa uso na ureno. Mabingwa wa kombe la dunia timu ya taifa ya Ujerumani imekubali kichapo cha goli 2-0 dhidi...
       Ufaransa uso kwa uso na ureno.









Mabingwa wa kombe la dunia timu ya taifa ya Ujerumani imekubali kichapo cha goli 2-0 dhidi ya timu ya taifa ya Ufaransa ambao ni wenyeji wa michuano ya mataifa ya ulaya mwaka huu.
Huu ulikuwa ni mchezo wa nusu fainali ya pili wakati nusu fainali ya kwanza ikifanyika hapo jana na kushuhudia timu ya ureno iliyoanza kwa kususasua kuibuka na ushindi wa goli 2-0 na kujihakikishia nafasi ya kucheza hatua ya fainali itakayochezwa siku ya jumapili hapo nchini ufaransa.
Pamoja na Ujerumani kuwa na kikosi bora walipoifunga timu ya Argentina mwaka 2014 katika fainali ya kombe la dunia, bado hawakuweza kufanya kitu mbele ya wenyeji wa mashindano hayo timu ya taifa ya ufaransa na hivyo ufaransa kuweza kulipa kisasi cha kufungwa na ujerumani katika hatua ya nusu fainali ya kombe la dunia lililofanyika huko nchini Brazil kwa gali 1-0.
Magoli ya ufaransa yaliwekwa kimyani na mshambuliaji wa kimataifa anayecheza katika klabu ya Atletical Madrid ya nchini Hispani akifunga goli la kwanza dakika ya 45+ kwa mkwaju wa penati na akikamilisha ushindi wa ufaransa dakika ya 72 na hivyo kuwatoa nje timu ya ujerumani waliokuwa wanapewa nafasi ya kutwaa kombe hilo.
Didier Deschamps ameendelea kumwamini Samwel Umtiti huku akimwacha nje beki wa kati anayekipiga katika klabu ya Sevilla Ardi Rami lakini pia kumwacha nje Ngoli Kante na kuwaanzisha viungo Paul Pogba pamoja na Bles Matuidi walioonyesha kuelewana sana katika idara ya kiungo.
Kihistoria katika mashindano makubwa kama haya ufaransa alikuwa hana matokeo mazuri sana lakini kwa ushindi huu, Ufaransa anapunguza lile gap alilokuwa amefungwa na ujerumani.

Fainali ya michuano hii itafanyika siku ya jumapili katika uwanja wa stade de massele ambapo wenyeji ufaransa watamenyana vilivyo na ureno timu iliyofika hatua ya fainali ikiwa kama best loser.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top