SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Paul Pogba, anakabiliwa na maamuzi magumu ama ajiunge na MU au la.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Paul Pogba, anakabiliwa na maamuzi magumu ama ajiunge na MU au la. Aliyekuwa kiungo mkabaji na nahohadha wa klabu ya Juvent...

Paul Pogba, anakabiliwa na maamuzi magumu ama ajiunge na MU au la.

Pogba (C) is likely to feature for France in their Euro 2016 final against Portugal




Aliyekuwa kiungo mkabaji na nahohadha wa klabu ya Juventus Alessandro Del Piero, amekubali ya kuwa Paul Pogba anakabiliwa na wakati mgumu juu ya maamuzi ya kuirudia tena klabu yake ya zamani Manchester United katika rekodi ya dunia ya paun 100m.
Pogba ambae anakabiliwa na mchezo wa fainali ya euro 2016 dhidi ya Ureno siku ya jumapili, aliondoka katika klabu ya Manchester kwa uhamisho huru, atarudi klabuni hapo kwa mshahara wa paund 300,000 kwa wiki?
Kwa sasa bado anamkataba na mabingwa wa Seri A, ambao unamweka klabuni hapo mpaka msimu wa 2019, na Del Piero anaamini vibibi vya Torino vitaendelea kumtumia kwa mwaka mmoja Zaidi.
‘‘Pogba ni mchezaji mkubwa, ana umuhimu mkubwa sana na tayari amekwisha onyesha kwa kila mtu,” Alisema Del Piero wakati akihojiwa na sky sport.
‘‘Sijui kinachokwenda kutokea, mazungumzo yamekuwa ni mengi mno, lakini nafikiri Juve wanahitaji kumtumia pogba angalau hata kwa mwaka mmoja, Lakini kwa bahati mbaya United ni klabu kubwa sana, lakini pia ni ngumu kwa yeye kuchagua wapi ni mahala sahihi kwake. Nikiwa kama Mwitaliano na mchezaji wa zamani wa Juve, natamani aendelee kuichezea Juve angalau hata mwaka mmoja Zaidi” Alimalizia Del Piero.

Lakini kiukweli maamuzi yote yapo kwa Pogba ni wapi atataka kwenda kucheza mpira wake akiwa bado kijana na ukiachilia mbali klabu ya Manchester United, pia Pogba anafukuziwa kwa ukaribu na Real Madrid ya nchini Hispania pamoja na mabingwa wa ligi kuu ya ufaransa Klabu ya PSG..

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top