
Timu nyingi za Africa ya Mashariki zimekuwa hazina matokeo
mazuri mbele ya timu kongwe katika mashindano mbalimbali kama vile kombe la
klabu bingwa barabi afrika, shirikisho lakini pia hata katika anga za
kimataifa, licha ya timu ya taifa ya Uganda, Uganda the Clames, kuendelea
kujikongoja katika hatua ya kutafuta tiketi ya kushiriki kombe la mataifa ya
Afrika ya mwakani, timu zote za ukanda wa mashariki, ndoto zao za kufuzu
michuano hiyo, zimekwisha yeyuka zamani.
Leo, tuangazie katika ngazi ya vilabu na haswa Zaidi,
tutaangalia nafasi ya klabu ya Young African katika mashindano ya shirikisho
yanayoendelea. Klabu ya Yanga kufuzu katika hatua ya makundi yaani robo fainali
ya kombe la shirikisho barani Africa, ilikuwa ni mwaka 1998 mwaka ambao pamoja
na kufuzu katika hatua ya makundi, bado Yanga hawakuweza kufanya vyema.
Katika michezo yote sita ya hatua ya makundi mwaka 1998 yanga
aliambulia pointi mbili pekee baada ya kutoa sare mbili na kuweza kufungwa
mechi zote nne.
Pengine ya kale yamepita, tuyaache na tugange yajayo. Hivi
huu msemo una maana yeyote? Kama ya kale yamepita, na yale makosa tuliyoyafanya
hatujifunzi ili tuje na kitu kipya? Mimi kwangu yakale huwa yanasehemu yake
katika kunitia moyo, kama nilikosea mahala, nitafahamu wapi nilipokosea ili
niweze kurekebisha, na kama nilifanya vyema nitatia juhudi ili nifanye vyema Zaidi.
Turudi kwenye mada yetu, Klabu ya Yanga pamoja na kwamba
ilihitaji makubwa tangu walivyopata nafasi ya kucheza katika hatua ya makundi,
bado mimi niliona si maana sana kwetu watanzania kujivunia nafasi, bali kwangu
ilikuwa ni sehemu ya kupata uzoefu ili, endapo tena Yanga wakajihakikishia
nafasi ya kucheza tena katika msimu unaokuja, basi mashindano ya mwaka huu
yangekuwa kama Platform katika kuhakikishisha wanatengeneza misingi bora ya kufanya
vyema.
Katika mechi tatu Yanga walizocheza wakiwa kundi A, wameweza
kupoteza mechi zao mbili kwa klabu ya MO Bejaia kwa goli moja na kukubali
kichapo kingine cha goli moja dhidi ya klabu ya TP Mazembe na kuweza kusuruhu
na klabu ya Medeama ya nchini Ghana.

Katika michezo mitatu aliyocheza yanga, miwili amecheza akiwa
katika uwanja wa nyumbani na mchezo mmoja akiwa ugenini huku raundi ya pili
akitaraia kusafiri kuwafuata Medeama, na TP Maezembe na kusaliwa na mchezo
mmoja hapa nyumbani.
Ni vigumu sana kupata matokeo katika viwanja vya ugenini hasa
kwa Kariba ya vilabu anavyocheza navyo Yanga. Uongozi wa klabu ya Yanga walikosea
kuwekeza nguvu nyingi kwa mashabiki ya kuwa wanakwenda kufanya vyema wakati
walikuwa wanajua kwa nadharia aina ya timu walizokuwa wamepangwa nazo, huku
kivitendo hatukuweza kukubali matokeo.
Na ndio maana hata ile kauli yangu ya kuwaasa mashabiki kutokupandikiza
akili ya ushindi kisha Yanga wakifanya vibaya, waonekane hawajui. Kwangu mimi
huu ni uzoefu wa hali ya juu ambao klabu ya Yanga wameupata kwa mwaka huu.Wana
kazi kubwa sana ya kuhakikishwa kile walichokuwa wanakiita ‘‘Tuna uhakika
tunakwenda kushinda, wakakifanya katika mashindano yajayo.”
Kwangu mimi naiita, Yanga walikwenda kushiriki kupata uzoefu,
na ndio maana hata sishitushwi na matokeo wayapatayo sasa.
Post a Comment