
Na charles Kunji.
Kocha mkuu wa klabu ya Manchester United Jose Morinho, ametambulishwa leo kuwa kocha rasmi wa mashetani wekundu siku ya jumanne na akisisitiza ya kuwa alikuwa ni mshindi kuamua kuirudisha klabu hiyo katika zama zake za kale.
Morinho mwenye umri wa miaka 53 raia wa ureno aliyebahatika
kuvifundisha vilabu vya chelsea, real madrid, pamoja na Inter milan, amesema
kuwa hahitaji kuona wachezaji wake wakiimarika wakiwa katika nafasi ya tano
mwishoni mwa msimu kama ni kitu chema.
'kwa mashabiki wa United, kwa miaka mingi, mafanikio yalikuwa ni
sehemu ya maisha yenu. Katika miaka mitatu iliyopita, ninahitaji msahau"
morinho aliwaambia waandishi wa habari.
'Sihitaji kuona wachezaji wakifikiri tunahitaji kufanya vyema.
Kwani nini maana ya kufanya vyema? Kumaliza msimu ukiwa nafasi ya nne?
Kwetu sisi kumaliza nafasi ya nne sio malengo yetu, Malengo yetu ni kushinda
taji"
'Nataka kila kitu, nataka kushinda mechi zangu zote, ninataka
kucheza vizuri, nataka kushinda magoli, sitaki kuruhusu magoli, ninataka kila
kitu" Morinho alifafanua.
Mchezo wa kwanza wa klabu ya Manchester United wakiwa chini ya
utawala wa Jose Morinho, utakuwa ni mchezo wa kirafiki dhidi ya klabu ya
Borrusia Dotimund katika kombe la binwa wa kimataifa litakalofanyika katika
uwanja wa Shanghai Julai 22. Mechi yao ya kufungua pazia ya ligi kuu ya
uingereza itakuwa dhidi ya klabu ya Bournamouth siku ya jumamosi tarehe 13
mwezi agosti.
Post a Comment