
Bastian Schweinsteiger, raia wa Ujwerumani
aliyeiongoza timu ya taifa ya Ujerumani kutwaa kombe la dunia mwaka 2014,
nafasi yake katika klabu ya Manchester United imekuwa ni ya mashaka tangu ujio
wa kocha mpya Jose Morinho.
Morinho amekwishafanya usajili wa wachezaji watatu
na anakaribia kukamilisha dili na kiungo wa timu ya taifa ya Ufaransa na klabu
ya Juventus Paul Pogba,
Bastian Schweinsteiger 31, anaonekana ni moja ya
list ya wale wachezaji 9 watakaotemwa na kocha huyo raia wa Ureno.
Schweinsteiger ambae ametangaza kustaafu soka la kimataifa, ameonekana akifanya
mazoezi akiwa peke yake wakati kikosi kamili cha United kikifanya nazoezi ya
jumla kwa siku ya kwanza.
Washambuliaji Adnan Januzaj, Will Keane na James
Wilson kiungo Andreas Pereira na mabeki Cameron Borthwick-Jackson, Tim Fosu-Mensah, Tyler Blackett na Paddy
McNair wameripotiwa kutafuta timu za kwenda kwa mkopo au kusajiliwa moja
kwa moja. Pamoja wachezaji wa kikosi cha kwanza kutokuwepo kwenye tour ya nchini
China, Schweinsteiger kutojumuika na wenzake katika mazoezi ya siku ya jana,
kunathibitisha rasmi ya kuwa huenda akaondoka klabuni hapo.
United inaripotiwa ililipa kiasi cha pauni
mil14.4 kupata kandarasi ya Schweinsteiger kutoka klabu ya Bayern Munich miezi
12 iliyopita lakini usajili huo haukufikia malengo na mkufunzi huyo.
Majeraha yalimfanya Schweinsteiger kucheza
mechi 31 pekee huku akikosa fainali saba ikiwemo ile ya FA United walipoifunga
Crystal Palace kwa ushindi wa goli 2-1. Alipata jeraha la goti katika
mashindano ya EURO ya mwaka huu alipoamua kustaafu kucheza timu ya taifa huku
akifunga goli 1 mechi walipocheza na timu ya taifa ya Ukraine.
Kocha wa sasa wa timu ya Manchester United Jose
Morinho anaonekana kutopendelea kutumia vijana haswa wale waliokuwa wanakuzwa
na kocha wa zamani wa klabu hiyo Louis Van Gaal ambae ameshindwa kuipa mafanikio
klabu hiyo.
Post a Comment