SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: ASTON VILLA YAENDELEA KUMNYEMELEA BRUCE.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
  ALIYEKUWA boss wa zamani wa timu ya Birmingham City, Steve Bruce ameendelea na mazungumzo na mabosi wa timu ya Aston Villa na ku...


 Steve Bruce

ALIYEKUWA boss wa zamani wa timu ya Birmingham City, Steve Bruce ameendelea na mazungumzo na mabosi wa timu ya Aston Villa na kuonyesha dalili za kuwa huenda akatangazwa kuwa kocha mpya wa Aston Villa baada ya kumtimua Roberto di Matteo siku ya jumatatu huku akiiacha klabu ikiwa nafasi ya 19 kwenye championship.

Bruce, 55, alikuwa hana timu yeyote kwa muda sasa japo alikuwa na interview ya kuitaka nafasi ya kuwa kocha wa timu ya England ambapo pia mipango haikumwendea sawa.

Msaidizi wa Di Matteo Steve Clarke ataendelea kubakia klabuni kama msaidizi na ataiongoza timu hiyo itakapokuwa na mchezo kwenye uwanja wa nyumbnai dhidi ya timu ya Wolverhampton Wanderers, 15 October.

Mchezaji wa zamani wa timu ya Birmingham, Robbie Savage, ambaye aliwahi kufundishwa na Bruce,  amemuelezea Bruce ya kuwa ni mtu sahihi wa kuja kuifundisha klabu ya Aston Villa.

"Steve Bruce amekuwa na mazungumzo ya kina Zaidi ya mara tatu ndani ya masaa 48 na wakuu wa Aston Villa, ingawaje bado ni kama wanauficha ukweli. Kililipoti kituo kimoja cha redio cha nchini England.

Hata hivyo, mazungumzo Zaidi na mmiliki wa klbau hiyo, bwana Tony Xia bado hayajaanza lakini wachambuzi wa masuala ya soka nchini huko wanaamini Bruce ni mtu sahihi wa kuiongoza klabu hiyo na hata kuirejesha ligi kuu.

Di Matheo amecheza mechi nane na hajapata ushindi hata mmoja atngu apewe timu hiyo.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top