SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: HLEB AIBEBESHA MATAJI KLABU YA ARSENAL MSIMU HUU.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
  MCHEZAJI wa zamani wa timu Arsenal, Alexander Hleb anaamini kwamba kikosi cha sasa cha Arsene Wenger kina uwezo wa kubeba mataji ...


 Image result for Alexander Hleb images

MCHEZAJI wa zamani wa timu Arsenal, Alexander Hleb anaamini kwamba kikosi cha sasa cha Arsene Wenger kina uwezo wa kubeba mataji matatu kwa mpigo msimu huu

Arsenal wamekuwa na matokeo mazuri katika michezo ya hivi karibuni, wakiwa na alama mbili nyuma ya vinara wa EPL, klabu ya Manchester City vilevile wakiwa wamejikusanyia alama nne katika michezo miwili kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Hleb ambaye wakati yupo Arsenal hakuwahi kushinda taji lolote anaona ubora wa sasa wa Arsenal ni wa kuchukua mataji matatu msimu huu.

“Naamini Arsenal watashinda mataji matatu msimu hu, ubingwa wa Premier League, Kombe la FA na Ligi ya Mabingwa pia,”Hleb amesema. ” Naiona Arsenal yenye uwezo na ari ya kupambana na kwa hakika nitaisapoti.”

“Mara nyingi Wenger huwa ana matarajio makubwa. Ameweza kuwabakisha wachezaji wake muhimu wote kwa sasa na wanacheza mpira mkubwa mno. Kila mpinzani wao lazima aingiwe na hofu!”

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top