SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: KOZI YA MAFUNZO YA MAKOCHA WANAWAKE KUFIKA TAMATI.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KOZI maalumu ya ukocha wa soka la wanawake imefikia tamati leo katika makao makuu ya shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF. Kozi ...



KOZI maalumu ya ukocha wa soka la wanawake imefikia tamati leo katika makao makuu ya shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF.
Kozi hiyo iliyoanza siku ya jumatatu, ilikuwa na lengo la kuinua soka la wanawake nchini ambalo linaonekana kutokuwa sawa tangu awali.

Akifunga kozi hiyo katibu wa shirikisho la mpira wa miguu nchini, TFF, Selestin Mwesigwa amesema makocha waliopata fursa ya kujifunza kozi hiyo wakaitumie ili kuinua soka la wamawake nchini.

“Tumewagharimia ili mje kusaidia soka la wanawake na sio kwenda kutundika vyeti hivi ukutani” Alisema Mwesigwa.

Aidha, katibu wa TFF aliongeza kuwa suala la vifaa bado lipo jikoni na hivyo makocha hao wawe na subra wanapotafutiwa vifaa hivyo kama vile jezi, mipira pamoja na vifaa vingine lukuki.

“Tunataka kuiomba serikali itusamehe kodi kwani kuna vifaa vingi ambavyo vipo bandarini na tunashindwa kuvitoa kwa sababu ya kodi” Alisema.
 Displaying KUNJII.jpg

Lakini pia mkufunzi wa kozi hiyo Bi Andrea, mwakilishi wa FIFA kutoka Mexico amefurahishwa na kozi hiyo ambayo imetolewa na shirikisho la mpira la Tanzania kushirikiabna na FIFA.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top