SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: mabingwa wa EPL wafanya usajili mwingine
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Leiceste r yamsajili Nampalys Mendy Na Charles Kunji Katika jitihada za kuhakikisha kikosi chao kinakuwa bora kabla ...

Leicester yamsajili Nampalys Mendy






Na Charles Kunji



Katika jitihada za kuhakikisha kikosi chao kinakuwa bora kabla ya kuingia kwenye harakati za kutetea taji lao, Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza Leicester City wamemsajili kiungo wa kati wa Ufaransa Nampalys Mendy.
Mchezaji huyo zamani akiichezea klabu ya Nice ametia sahihi kandarasi ya miaka minne kufanya shughuli nchini Uingereza.
Hata hivyo, Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 hajawahi kuitwa katika kikosi cha taifa cha Ufaransa.
Akiongea wakati anakaribishwa klabuni hapo, mendi alisifu ubora wa klabu hiyo lakini pia na mkuu wake wa kazi mpya.
'Namfamu kocha, nafahamu uwezo wake lakini pia nafahamu falsafa yake natumai nitafanya kazi."  aliongea hayo Mendy
Mendy alijiunga na Nice mwaka wa 2013 akitokea klabu ya Monaco alikoichezea katika mechi 110 za ligi ya daraja ya juu Ligue 1 katika misimu 3.
Mendy ni mchezaji wa tatu kujiunga na mbweha wa jangwani   baada ya kipa Ron-Robert Zielerand na mlinzi Luis Hernandez.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top