SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: VIDEO; GOLI LA DAKIKA YA 89 LILILOWATOA UGANDA AFCON
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
USIKU wa January 21 2017 wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika Mashariki katika michuano ya mataifa ya Afrika maarufu kama   AFCON 201...
Abdallah El Said



USIKU wa January 21 2017 wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika Mashariki katika michuano ya mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON 2017, timu ya taifa ya Uganda ilitolewa rasmi katika michuano ya mataifa ya Afrika yanayoendelea nchini nchini Gabon.

Uganda wameaga mashindano hayo baada ya kukubali kipigo cha goli 1-0 dhidi ya mabingwa mara 7 wa kombe hilo, timu ya taifa ya Misri katika mchezo wao wa pili wa Kundi D.

Uganda wanaaga mashindano hayo na kuwa wanasubiria mchezo wao wa kukamilisha ratiba dhidi ya Mali, ukiwa ni mchezo wa kukamilisha ratiba ambapo hata wakishinda bado hawataweza kufuzu kuendelea na michuano hiyo

Abdallah El Said wa Misri ndio alihitimisha safari ya Uganda katika michuano ya AFCON 2017, baada ya kufunga goli dakika ya 89 kwa kutumia vyema assist iliyotolewa na Mohamed Salah.

Hata hivyo kulingana na rekodi za kwenye makabrasha, Uganda ni timu dhaifu mbele ya Misri, kwani leo wanakuwa wamefungwa kwa mara ya 16 na mara ya mwisho Uganda kuifunga Misri ilikuwa 1965 katika michuano ya kama hiyo.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top