
MAPINDUIZ cup imefikia patamu ambapo leo kutakuwa na michezo ya nusu
fainali ikifanyika huku macho na masikio ya mashabiki wengi ni kuiona ile dabi
ya Kariakoo yaani Simba vs Yanga.
Hawa ni watani wa jadi
wa soka la hapa bongo na leo katika nyasi za uwanja wa Amaani mjini Zanzibar,
ni dakika 90
ama 120 za mwamuzi
ndizo zitakazoamua ni nani ataweza kuibuka na ushindi.
Nusu fainali ya kwanza
itawakutanisha wababe wa Zanzibar, Taifa Jang’ombe watakaocheza na mabingwa wa
Africa mashariki na kati, timu ya Azam wakati dabi ya Kariakoo itakuwa saa
mbili usiku.
Maoni yako ni ya
muhimu sana kueleka mtanange huo utakaokuwa wa vuta nkubute.
Post a Comment